Wednesday 3 October 2012

VITA VYA majimaji “MACHINJIO” YA WAISLAMU


Nje kidogo ya mji wa Songea kuna kitongoji kinaitwa Mahenge,hapo kuna sehemu ya kumbukumbu ya vita vya Majimaji.

Jambo kubwa la mahala hapo ni Kaburi kubwa la halaiki ambamo askari zaidi ya sitini na….
walizikwa kwa pomoja.Na kando ya kaburi hilo la pomoja kuna kaburi la Ally Songea Mbano ambae yeye alizikwa peke yake.

Kwa mara ya kwanza nilitembelea makumbusho hayo mwishoni mwa mwaka 2007.

Baada ya kusaini kitabu cha wageni,na kulipa ada ya kituo,muhudumu wa kituo hicho alitupa karatasi yenye orodha ya majina ya wale wote walionyongwa na kuzikwa hapo.

ukiitazama orodha hiyo na hasa ukiwa mwislam jambo moja litakustuwa.Robo tatu ya walionyongwa na kuzikwa hapo ni waislaam .

linaanza jina lake la kiiislam, kisha kwenye mabano kuna jina la Kikristo na mwishoni linaishia jina la kiasili, mfano Abdulrahman[Dominic]Mputa Gama.

Muhudumu akatueleza kuwa hawa mashujaa wa vita vya majimaji kabla ya kunyongwa alikuwako padri ambae aliwabatiza na kuwapa majina ya kikristo na baadae kunyongwa,wengi walibatizwa kwa hadaa kuwa wakibatizwa wataachiwa huru,wote katika hao walionyongwa walikuwa ni waislam.

Uzuri ni kwamba katika orodha hiyo kulikuwa na jina na sahihi ya Yule padri aliyewabatiza, na kwa mkono wake[huyo padri] aliiyaandika hayo majina.

Karatasi yenyewe ilihifadhiwa vizuri kwenye fremu ngumu ya kioo.Tuliomba kwa nguvu zote kupatiwa hiyo karatasi ya majina hata kwa kununua lakini haikuwezekana pamoja na kuwaona wakubwa wa kituo hicho.

Niliporudi kwa mara ya pili mwezi July 2009.nilipata mstuko.

Karatasi iliyohifadhiwa kwenye fremu ngumu ya kioo,iliyokuwa na majina ya Kiislaam ya mashujaa wa vita vya majimaji,haikuwapo,na badala yake imewekwa karatasi nyingine ombayo ndani ya karatasi hiyo majina ya kiislaam ya mashujaa hao wa vita vya majimaji yameondolewa na kuachwa majina ya ubatizo na yale ya kiasili tu,jina la padri,sahihi yake na wadhifa wake katika kanisa katoliki pia vimeondolewa,na karatasi yenyewe haikuwa kwenye fremu ya kioo na ilikuwa katika fotokopi tu.

Nilimuuliza Muhudumu kulikoni? Akasema……. Songea pana mzee mmoja maarufu sana katika historia ya Tanu na historia ya kuasisiwa Bakwata anaitwa kwa kifupi M.S. Mzee huyu ana binti yake ambaye ameolewa na mzungu wa kijerumani.

Binti huyu na na mumewe wa kijerumani walikuja hapa Songea matembezi.

Hivyo kwa shinikizo la huyu mzee M.S. karatasi hiyo alipewa huyu mzungu kwa ahadi kwamba anaipeleka Ujerumani na atairudisha.

Hivyo ndio karatasi ile asilia ilivyotoweka. Kubwa katika karatasi ile ni ule ushahidi wa majina kuwa wote katika wale walionyongwa na kuzikwa hapo ni waislaam,wengi katika hao walihadaiwa kuachwa huru hivyo wakabatzwa ispokuwa wachahe sana waligoma kama shujaa Ally Songea Mbano.

Huyu kwa ushujaa wake wa kupambana na Wajerumani aligoma na akasumbua sana kiasi akanyongwa siku yake na peke yake na ndio sababu akazikwa pia peke yake.

Ukiingia ndani ya kinyumba cha ghorofa,unaanza kuona picha za mashujaa wa majimaji wakiwa wamevaa mavazi ya vita mithili ya mahujaji wanavyovaa Ihraam wakati wa hija.

kinachoongezeka kwao ni vilemba kichwani.Chini ya kila picha kuna jina la mwenye picha.Katika picha hizo majina Ukipanda gorofani utaona silaha za kijadi,mikuki,pinde,mishale,ngao,n.k.

Kinachosisimua zaidi ni mavazi ya vita.mavazi ya vita ya askari wa majimaji wengi walivaa kanzu za kiislaam na vilemba.

Jambo jingine linalosisimua ni kile ambacho watu wa kituo hicho wameandika”Rosary”[hili ni jina la kikristo,hasa la kikatoliki,ni zile shanga ambazo huning’inia msalaba]lakini unapotazama hicho kilichoitwa “Rosary” utaona si Rosary, bali ni Tasbihi hasa ya kiislaam yenye kupangika hasa shanga zake,33,33,34.maneno yaliyoandikwa kuelezea Rosary hizo ambazo ni Tasbihi ni “Hizi ni Rosary ambazo wapiganaji wa majimaji walikuwa wakitumia KUTAMBIKA kabla ya kwenda vitani kwa kuamini kwamba zitawakinga na risasi.

ukweli ni kwamba hawa askari wa majimaji wengi walikuwa ni waislaam hivyo hawakuwa WAKITAMBIKA bali walikuwa wakitumia Tasbihi hizo kufanya Dhikri kwa Allah kabla ya kwenda vitani.

Midhali sisi waislaam hatujawa tayari kuandika historia yetu kama waislaam,wanaotuandikia watapotosha na kupindisha na kutuzulia wanavyotaka.

Hapo gorofani kuna jingine la kasisimua.kuna makopo au magudulia.

Wameandika kuwa,haya ndio makopo ambayo askari wa majimaji walikuwa wakiyatumia KUNAWA kabla ya kwenda vitani[kushika udhu na sio kunawa]pia kwa kuamini kuwa maji hayo yatawakinga na Muhudumu alitueleza kuwa kumbukumbu nzuri na za uhakika ziko Jimbo kuu la Wakatoliki,Peramiho.

Tulikwenda jimboni lakini hatufanikiwa kwa sababu za ki-urasimu tu.Tulitakiwa tupate kibari cha Askofu mkuu.Hatukukipata.

Kwa yale tuliyoyaona na kuyashudia tulijifunza mambo yafuatayo:-

1.Vita vya majimaji havikuwa ni vita vya kizalendo, kwamba wazalendo walikuwa wakipigania nchi yao.La!!!Vilikuwa ni vita vya waislaam wakipigana na wakristo wa kijerumani waliovamia maeneo asilia ya waislaam kwa lengo la kuuwa uislaam na kusimamisha Kanisa.kwani mazingira yote utayoyaona ya mashujaa wa vita vya majimaji ni mazingira ya kiislaam,kingine ni kwamba hukuti mahala yalipo makaburi ya askari wa kijerumani ila katika miji ya waislaam.Kilwa.Bagamoyo.n.k.kwa nini wauliwe maeneo ya waislaam tu?walifuata nini huko?

2.kuna upotoshaji mkubwa sana wa historia ya vita vya majimaji.Vinaoneshwa kama ni vita vya wazalendo wakipigana na wakoloni wa kijerumani,wakati ukweli si hivyo.Ukweli ni kwamba vita vya majimaji vilikuwa ni vita baina ya waislaam na wakrito wa kijerumani,waafrika wakristo wa songea walijiunga na wakristo wenzao wa kijerumani dhidi ya waafrika wenzao wa kiislaam.

3.Wakristo wameitafiti hakika hii na wakaijua kisha wameificha kwa maslahi yao. MWISHO Kuna haja ya wasomi wetu wa kiislaam kufanya juhudi za makusudi za utafiti wa Historia yetu ili kukifanya kizazi hiki cha kiislaam kujitambua zaidi na kujenga ujasiri.Taasisi za kiislaam na watu binafsi[matajiri]wawawezeshe kiuchumi wasomi hawa kufanya kazi hii.

Mwaka 2008 nimetembelea Kilwa kisiwani ,huko nikamkuta mzungu wa kifaransa akiandika historia ya kilwa kisiwani akiitwaThiery,ameweka kambi na majenereta ya umeme,solar power,na makompyuta.kazi nyingine kubwa alokuwa akifanya ni kukarabati yale magofu ambayo mengi ni Misikiti na majumba ya mawe ya wafalme wa kale.

Kilwa kisiwani ni moja kati ya dola kubwa za kiislaam katika mwambao wa Afrika mashariki,ndio dola ya mwanzo kuwa na sarafu yake ambayo iliandikwa jina la Allah.

Tuliposoma kazi ile ya Yule Thiery mfaransa tayari alikwisha ipotosha kwa kiasi kikubwa.sikuwa na la kumfanya.Kizazi cha vijana wa kiislaam hakitopata historia ya kweli ya kiislaam kama tutawaacha akina Thiery waandike,na hivyo vijana wetu hawatajitambua na hawatokuwa na ujasiri katika uislam wao.

Sunday 26 February 2012

FAIDA YA TAQWA (Ucha Mungu)

Anasema Allaah سبحانه وتعالى

((... وَمَن يَتَّقِ اللَّهَ يَجْعَل لَّهُ مَخْرَجًا )) (( وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لاَ يَحْتَسِبُ ..))

((Na atakayekuwa na taqwa (kumcha Allaah) Humtengezea njia ya kutokea)) ((Na Humruzuku pasinakutegemea)) [At-Twalaaq: 2-3]

Hizo ni kauli za Allaah سبحانه وتعالى katika Kitabu Chake Qur-aan Tukufu, ambayo ni Uongofu kamili wa mwanaadamu.
Kitabu kisichokuwa na shaka wala kufikiwa na ubatilifu mbele yake wala nyuma yake, kimeteremshwa na Mwenye Hikma Ahimidawaye.

Taqwa ni wasiya wa watu wa mwanzo na wa mwisho, na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliwausia Maswahaba wake wapenzi :

عن أبي ذَرٍّ جُنْدُب بِن جُنَادَة، وأبي عبد الرحمن مُعَاذ بِن جَبَلٍ رضي الله عنهما، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: ((اتق الله حيثما كنت، وأَتْبِعِ السَّيئةَ الحسنةَ تَمْحُها، وخالقِ الناسَ بخُلُقٍ حسنٍ)). رَوَاهُ التِّرْمِذِيُّ .

Kutoka kwa Abu Dharr Jundub Ibn Junaada na Abu Abdur Rahmaan Mu'adh Ibn Jabal رضي الله عنهما ambao wamemnukuu Mtume صلى الله عليه وسلم akisema: ((Mche Allaah popote pale ulipo, na fuatisha kitendo kibaya kwa kitendo kizuri kitafuta (kitendo kibaya), na ishi na watu kwa uzuri))

Na Taqwa haihitajii kuhakikishwa kuwa mahali fulani au wakati fulani, bali taqwa ya hakika ni pale mtu anapokua yuko peke yake, akajiepusha na yaliyo haraam japokuwa hakuna mtu anayemuona.
Na ndipo aliposema Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kuwa 'Taqwa iko hapa' akiashiria kwenye kifua chake palipo na moyo na kusema mara tatu.

Thursday 23 February 2012

Vipi Tunaweza Kufaidika Na wakati?
1. Kukumbuka kifo na misukosuko yake.
2. Kujizowesha kuthamini wakati na umuhimu wake katika kutekeleza ahadi.
3. Kukumbuka jambo gani muhimu la kufanya ili upate radhi za Allah.
4. Kuihesabu nafsi yako kuwa umefanya lipi la kumridhisha Allah.
5. Kukumbuka mwisho wa kila jambo baya na adhabu itakayomkabili kila mwenye kutumia wakati kwa kufanya maovu.
6. Kukumbuka wasia na mafundisho ya Mtume s.a.w juu ya kufanya matendo mema na malipo yake.
7. Kuandaa muongozo au ratiba ya kuendeleza mambo yako ya kila siku ambayo ni msingi katika maisha.
8. Kujiepusha na tabia ya kusahau.
9. Kushiriki katika mambo muhimu ya jamii na kutoa kila unachoweza kutoa kwa ajili ya kuisaidia jamii, kwani utaja ulizwa siku ya masiku kuwa umetanguliza kitu gani katika vitu alivyokujaalia Allah juu ya jamii uliyokuwa unakaa.
10. Kusoma vitabu mbali m bali vya mafundisho ya dini kujua kuwa Mtume s.a.w pamoja na msahaba na watu wema waliyokuja baada ya Mtume s.a.w na masahaba zake kujua walikuwa wanafaidika vipi na wakati.
11. kuwa na mazoeya ya kusoma kitabu kitakatifu cha Allah wakati ambao upo katika kusubiria kitu au usafiri (kituoni) au ndani ya chombo cha usafiri ukiwa katika safari ndefu, ili mradi usikubali kupitwa na neema hii ya wakati.
12. Tufahamu kuwa wenzetu wanafanikisha vipi mambo yao kwa kuchunga wakati, hasa hasa makafiri, kwani hujulikana kuwa ni watu wenye kuzingatia sana wakati kuliko hata tulivyo sisi ambao Mungu ametuletea muongozo wa mitume na vitabu vitukufu vyenye kila m uogozo wa maisha yetu, lakini kwa masikitiko makubwa sisi ndio watu wa mwanzo katika kupoteza neema ya wakati na kusahau thamani yake.

Allaah tumuombe atujaaliye tuwe watu wa kuthamini wakati.

Wednesday 1 February 2012

SOMO LA TAREKH (DARASA LA KWANZA

MBINU ZA KUFUNDISHIA
• Mwalimu ataje majina ya Mitume 25 na kuwataka wanafunzi wamfuatishe.
• Aorodheshe majina 25 kwenye ubao na kuwaamuru wanafunzi kuandika.
• Asisitize kwa wanafunzi kuwa Mitume wote wamekuja kufundisha Uislamu.

VIFAA VYA KUTUMIA
Vitabu vya Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) na vitabu vya visa mbali mbali za Mitume ya Allah.

LENGO.
Afahamu kuwa Mitume wote wamekuja kufundisha Uislamu.
Mtume wa Allah Muhammad(S.A.W.) kuwa ni Mtume ni Mtume wa mwisho.
KWA NINI UISLAMU UMEHARAMISHA WANAUME KUVAA DHAHABU NA HARIRI?

Leo ulimwenguni kote kutokana na kile kinachojulikana kama wimbi la kwenda na wakati, uhuru na haki ya mtu kufanya/kuishi atakavyo; si jambo la kushangaza wala kustaajabisha kuwaona vijana wa kiume wakiwa wamejipamba kwa kuvaa mikufu, pete na hata hereni za dhahabu.
Hili leo si geni tena bali ni jambo la kawaida na fakhari hata katika miji ya mwambao wa Pwani ya Bahari ya Hindi, ambako asilimia kubwa ya wakazi wake ni wafuasi wa dini ya Kiislamu kwa miongo ya miaka.
Uvaaji huu wa dhahabu kwa vijana wa kiume umeingizwa pande zetu hizi za Afrika ya Mashariki na vijana waliotoka huku kwenda nchi za Ulaya kutafuta ajira hasa ya ubaharia. Hawa waliporejea wakiwa wameuiga utamaduni huo wa kigeni na kuwaathiri vijana wengine, limbukeni wenye kuiga kila kiingiacho mjini.
Utamaduni huu wa vijana wa kiume kujipamba kwa kuvaa dhahabu unakwenda kinyume na utamaduni wa mila ya Kiislamu.
Mwenyezi Mungu amemuumba mwanamume na Mwanamke na kumpa kila mmoja maumbile na tabia zinazotofautiana na mwenzake. Ikiwa hili linaashiria kitu, basi si kingine bali ni kutofautiana pia katika nafasi na majukumu ya kila mmoja wao. Nadharia inaonyesha kuwa tabia na maumbile ya mwanaume ni ukakamavu na ugumu, wakati ambapo tabia na maumbile ya kike ni ulaini na ulegevu.
Uislamu unamtaka mwanaume alelekee katika mazingira yaliyo mbali na udhaifu,unyonge na anasa zinazoweza kunlegeza ili aweze kuwa imara na mwenye nguvu katika kupambana na harakati za maisha ya kila siku, ambapo sehemu kubwa ya jukumu hilo amebebeshwa yeye na sheria .
Sasa kwa kuzingatia kuwa madini ya dhahabu na hariri ni vitu vya anasa ambavyo humfanya mvaaji aonekane amependeza machoni mwake yeye mwenyewe kwanza na machoni mwa wengine na natija yake ni kuvaana na maumbile ya kupendeza ambayo ni ulaini na ulegevu.
Pengine kwa njia moja au nyingine hii ndio inaweza kuwa hekima/falsafa ya kuharamishwa dhahabu na hariri kwa wanaume kwa kuwa inakubaliana na tabia na maumbile yao. Hebu tujaribu kuwa wakweli, tuwatie katika mizani ya haki na uadilifu wanaume wenye kuvaa dhahabu na wasiovaa dhahabu, tutagundua nini? Bila ya shaka mtakubaliana na mimi kuwa ipo tofauti ya dhahiri baina yao, wavaao dhahabu watakuwa wameathirika na tabia na maumbile ya kike.
Taathira hii utaiona katika mwendo wao, uzungumzaji wao, uvaaji wao na wakati mwingine huiga hasa tabia za kike kama vile kusuka nywele na kutumia vipodozi.
Ni kweli usiopingika kwamba kujua hekima/falsafa ya kuharamishwa dhahabu na hariri kwa wanaume, hii ni elimu isiyo na manufaa na ni ujinga usiodhuru.
Usiulize hekima kwa kuwa kumeshurutishwa katika kuulizia hekima ya amri au makatazo, awe huyo muamrishaji/mkatazaji analingana sawa na kufanana na huyo muamrishaji/mkatazwaji na hapa ni suala la Mungu Muumba Muamrishaji na mwanadamu kiumbe muamrishwa. Kwa mantiki hii mwanadamu hana budi kuikubali na kuipokea amri kwa kuwa Mola wake ameamrisha/amekataza,kisha baada ya kutekeleza aliloamrishwa ndipo anaweza kutafuata kujua hekima/falsafa ya amri ile.
Lakini kule kujua hekima/falsafa iliyomo katika amri au katazoisiwe ni sharti ambalo kwanza ni lazima litimizwe kabla ya kuamrika au kukatazika. Muislamu wa kweli anaambiwa na Mola wake:
“HAIWI KWA MWANAUME ALIYEAMINI WALA KWA MWANAMKE ALIYEAMINI, ALLAH NA MTUME WAKE WANAPOKATA SHAURI,WAWE NA HIARI KATIKA SHAURI LAO. NA MWENYE KAMUASI ALLAH NA MTUME WAKE, HAKIKA AMEPOTEA UPOTOFU ULIO WAZI (kabisa) [33:36]
Kuharamishwa uvaaji wa dhahabu kwa wanaume kumethibiti katika hadithi nyingi sahihi zilizopokelewa kutika kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu –Rehema na Amani zimshukie.

1. Amepokea (riwaya) Imamu Bukhaariy, Muislam na Ahmad kwamba Mtume wa Allah “Amekataza (kuvaa) pete ya dhahabu”.
2. Imepokelewa kutoka kawa Ibn Abbaas-Allah awawiye radhi-kwamba Mtume wa Allah aliiona pete ya dhahabu kidoleni mwa mtu, akamvua na kuitupa (huku) akisema “ Mmoja wenu analikusudia kaa la moto na kulivaa mkononi?” Mtu yule akaambiwa baada ya kwenda zake mtume “ Itwae pete yako unufaike nayo. Akawajibu Wallah hapana, kamwe sitaichukua ikiwa aliyeitupa ni Mtume wa Allah –Rehema na Amani zimshukie.” Muislam.
3. Na katika jumla ya riwaya zilizopokelewa kwamba Mtume wa Allah –Rehema na Amani zimshukie amesema : “ Ye yote mwenye kumuamini Allah na siku ya mwisho basi asivae hariri wala dhahabu.” Al-musnad {Musnadul–Imam Ahmad}

Tuesday 31 January 2012

NAMNA YA KUPANGILIA WAKATI:

Kupangilia wakati ndio njia ya mafanikio. Vitabu vya dini vinahimiza watu wawe na ratiba ya mambo ya ibada na mengineyo. Mtu asiye na ratiba hana mafanikio maishani vyovyote atakavyokuwa.
Kwani kujipangia ratiba ni sawa na methali ya Kiswahili isemayo “Mali bila ya daftari hulika bila habari” wakati ni mali, na mtu asiye na ratiba mara nyingi hupoteza wakati mwingi bila habari! Ukijiwekea ratiba nzuri itakusaidia kutekeleza mambo yako kwa ufanisi. Lengo la kurasa hizi ni kutoa mwongozo juu ya namna ya kujipangia ratiba ya kila siku.

NAMNA YA KUPANGA RATIBA.
1) Kwanza kabisa, fahamu kile unachokihitaji kukitenda kwa siku nzima. Kisha jipe muda maalum wa kukamilisha kila tendo.
2) Jaribu kuweka uwiano mzuri (balanzi) yaani jipe muda wa kutosha kwa ajili ya kazi, mapunziko, kutazama TV, kuongea na marafiki, kupiga soga katika utandawazi, kufanya mazoezi, muda wa ibada, kutembelea ndugu, nk.
3) Kwa muda wa kujifunza, jaribu kuupangia ratiba katika nyakati ambazo unakuwa mchangamfu na hakuna vishawishi kama mechi za soka, michezo ya kuigiza, na kitu chochote upendacho kukifanya kwa wakati huo.
4) Jitahidi utenge muda wa kujifunza takriban kila siku, chagua muda kwa kila siku wa kujifunza sio mbaya kama kutakuwa na mapunziko siku moja au mbili kwa wiki.
5) Kila siku jipe muda huru usio wa kufanya kitu chochote, ndani ya muda huo waweza kufanya lolote bila kudhuru maslahi yako.
6) Jilazimishe kufuata ratiba yako.

NAMNA YA KUJIANDAA NA MTIHANI.
Maandalizi bora kabla ya mtihani ni kujisomea kwa njia zinazoleta matunda mazuri. Na zifuatazo ni baadhi ya njia zinazoweza kuleta mafanikio katika mitihani:
1. Jiandae mapema kwa ajili mtihani.
2. Jisomea kila siku kwa mujibu wa ratiba.
3. Ikiwezeakana jisomee na wenzako (weka kambi ya mtihani).
4. Pitia vizuri masomo yote.
5. Hakikisha unapata muda wa kutosha wa kupunzika ili usipate kihoro au homa ya mtihani.
6. Kula vizuri, fanya mazoezi ya mwali ili uwe mchangamfu.
7. Usiku wa mtihani jisomee kwa muda wa masaa yasiozidi matatu, kisha pumzika vizuri na ulale kiasi cha kutosha.
8. Fika mapema katika chumba cha mtihani, robo saa kabla ya kuanza mtihani.
9. Soma vizuri karatasi ya mtihani kwa ukamilifu, na jaza sehemu husika kama inavyotakikana. Usisahau, kuandika namba ya mtihani, jina, tarehe na mambo yote muhimu.
10. Hakikisha unasoma maswali kikamilifu na kuyaelewa vizuri na kama hujayaelewa muulize msimamizi akupe ufafanuzi.
11. Anza kujibu maswali mepesi kabla ya magumu, kama taratibu za mtihani zinaruhusu kufanya hivyo.
12. Baada ya kumaliza kujibu maswali yote, tafadhali yapitie majibu yako yote kwa ukamilifu.
13. Usiwe na pupa ya kutoka nje ya chumba cha mtihani.
14. Soma kwa mara ya mwisho majibu yako,na utakapokuwa na uhakika ya ulichokiandika peleka karatasi yako kwa msimamizi wa mtihani na tia saini ya kuhudhuria.
NAMNA YA KUISHUGHULIKIA MISAMIATI MIGUMU:

Kwa hakika wanafunzi wa kigeni (yaani wale wanaojifunza kwa lugha zisizo za asili yao) wanakabiliana na changamoto za maneno magumu. Ili kujaribu kutatua tatizo hili, karatasi hizi zimejaribu kuanisha baadhi ya njia za kumsaidia mwanafunzi aweze kutatua tatizo la misamiati migumu kwa upande wake. Kwanza kabisa kabla ya kuelezea namna ya kupata maana za maneno magumu tunapenda tuzingatie yafuatayo.

MAMBO YA KUZINGATIA:
1. Usipendelee kutafuta maana ya maneno magumu katika kamusi kwani kamusi linaweza kukukatiza katika kusoma kwako. Tafadhali jaribu kutumia muktadha wa maneno (mtiririko wa tungo/sentesi) kujipatia maana ya maneno magumu kwani hilo litakusaidia kuendelea na kusoma bila kukatisha.
2. Unapopata maana ya neno kwa kupitia muktadha wa maneno, tafadhali liweke alama kisha, ukimaliza kusoma, litazame hilo neno katika kamusi na ulinganishe maana uliyoipata na ile ya katika kamusi. Kama itawezekana tumia kamusi maalum za istilahi za somo husika.
3. Kama hukufanikiwa kupata maana ya neno kupitia njia ya muktadha wa maneno, hapo ndipo unapotakiwa kutumia kamusi. Baada ya kuona mazingatio haya, sasa tutazame njia za kupata maana ya maneno magumu.

A: Njia za kupata maana ya maneno magumu:
I. Kwanza liwekee alama neno gumu kisha soma aya/ibara nzima hapo unaweza kupata maana yake. Na kama hujaipata, jaribu kuendelea na kusoma huenda maana yake ukuipata katika mistari ya mbele.
II. Kutumia kamusi. Ukiwa umeshindwa kabisa kupata maana ya neno kutokana na maelezo yaliyoandikwa katika kitabu husika, tumia kamusi kwa umakini, kwani mara nyingi kamusi inatoa fasili mbalimbali za neno husika.

B: Kupata maana ya neno kwa kupitia viashirio vya muktadha:
I. Wakati unasoma kitabu kwa lugha ya kigeni kisha ukakumbana na neno gumu, njia sahihi ya kutambua maana ya neno hilo ni kwa kupitia viashirio vya muktadha wa maneno.
II. Na muktadha wa maneno maana yake ni mazingira ya neno katika tungo au sentesi yenye kuonesha uhusiano wake na maneno mengine. Kwa Mfano neno meza kwa wale wasio waswahili, likitokea katika sentesi kama hii:
Tafadhali usikae juu ya meza. Hapa muktadha unaanisha kuwa neno meza hapa lina maana ya nomino (jina) la samani/fanicha iitwayo meza. Wala halina maana ya meza kitenzi (kitendo) cha kula na kumeza kitu kinacholiwa.
III. Viashirio vya muktadha wa maneno maana yake ni maneno mengine yaliyopamoja na hilo neno gumu katika tungo. Tukichukulia mfano uliopita utaona maneno usikae juu ya yanaashiria samani/fanicha. Wala hayaendani na neno meza kwa maana ya kumeza chakula.

AINA ZA MUKTADHA WA MANENO.
Fasili:
Wakati mwingine sentesi zinatoa fasili ya neno gumu. Mfano: ukikuta imeandikwa Kompyuta ni mashine ya umeme inayohifadhia na kuchanganua taarifa zilizoingizwa. Kwa hakika hii si fasili ya kamusi lakini inakupatia maana na matumizi ya hilo neno kwa hapo lilipo.
Mifano:
Wakati mwingine neno gumu linafafanuliwa kwa kupigiwa mfano ambao unaweza kukupatia maana ya neno husika. Mfano: Kipa wa Ruvu staa apunguze mbwewe, kama za kuchezacheza na mpira katikati ya mstari wa goli, na kujifanya hakuuona mpira, kudaka kwa mkono mmoja na kujifanya kateleza.

Ufafanuzi:
Kutoa maelezo ya neno husika. Mfano: Mwanafunzi mchecheto, yaani yule anayejikojelea kwa kuhofia mtihani anapaswa apewe ushauri nasaha.
Visawe: (mutaraadifaatu/sinonim)
Kisawe ni moja kati ya maneno mawili au zaidi yanayokaribiana sana kimaana. Mfano: Inasemekana huyo Mwizi hakutambua au hakujua kama nyumba ile inalindwa kwa kamera maalum.

Kwa ibara nyingine:
Ibara ni kifungu cha maneno au habari iliyokamilika, mfano: Tume ya haki za binadamu imefichua nyeti za mauaji ya kimbari, kwa kuziweka wazi siri za mauaji hayo.

Vinyume:
Kinyume ni neno lenye kukinzana na neno lingine. Mfano: mtu mwenye huzuni hana furaha hata kidogo.

Kutafakari:
Watu wengi wanapata kihoro wanapokutana na simba mbugani. Mtu anayetatafakari sana anaweza kujua maana ya kihoro kwa ktazama muktadha wa tungo hii.
Pia unapaswa kuzingatia muktadha wa neno wakati unapotazama fasili yake kutoka katika kamusi.
Na kama hujapata maana ya neno tafadhali litazame katika katika kamusi.