Sunday, 25 December 2011
Mashairi: Siku Macho Nikifumba (Sisitizo)
Twaha H. M Kiobya [Mujaahid]
TIOT Morogoro
 1.  Bismillah naanza, kwa jina la utukufu
        Nia watu kuwafunza, Natumia hii safu
         Niepushe ya kuponza, wafanye uadilifu
               Hayatasaidia wafu, Masadaka ya matanga
 
 
          2. Uloyatenda mwenyewe, kabla ya kutawafu
Mazuri au yasiwe, atakulipa Raufu
           Hata kama usomewe, mahitaji maradufu
Hayatasaidia wafu, ma-sadaka ya matanga
 
3. Wale nyama au sunga, hayafuti ulanifu
                   Hawawezi pata mwanga, wale washibe wakinifu
        Haya ninyi mwajivunga, tatu hazifiki wafu
           Hayatasaidia wafu, ma-sadaka ya matanga
 
4. Ni uzushi kwenye dini, hajasema Ashrafu
           Si kitu arobaini, utapooza minofu
          Wale wakudanganyeni, ma vyakula na sarafu
       Hayatasaidia wafu, ma-sadaka ya matanga
 
 
5. Msimbe hayo yashike, mshairi maarufu
    Kwenye uzushi utoke, ufate wasadikifu
  Usingoje uumbuke, ya uzushi ni uchafu
          Hayatasaidia wafu, ma-sadaka ya matanga
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment